IQNA

14:54 - November 21, 2011
Habari ID: 2226169

Kikao kikubwa zaidi cha banki za Kiislamu duniani chaanza Bahrain

Washika dau katika sekta ya mfumo wa kimataifa wa benki na taasisi za kifedha za Kiislamu wanakutana katika Mkutano wa 18 wa Kila Mwaka wa Benki za Kiislamu (WIBC 2011) kuanzia Novemba 21 nchini Bahrain.

Akizungumza kabla ya kuanza mkutano huo wa siku tatu, David McLean mkurugenzi wa Mkutano wa Benki za Kiislamu amesema, 'katika miaka ya hivi karibuni mfumo wa kifedha wa Kiislamu umeimarika na kustawi kwa kasi katika kutoa huduma bora kimataifa'.
Amesema kongamano la mwaka huu litajadili 'Mashindano kwa ajili ya Ustawi wa Dunia' lengo likiwa ni kuimarisha kiwango cha mfumo wa Kiislamu wa fedha kote duniani. Amesema mkutano wa mwaka huu unahudhuriwa na wawakilishi kutoka nchi 50 duniani.
902264
captcha