IQNA

16:26 - November 29, 2011
Habari ID: 2231413

Lengo la kuwekewa vikwazo Syria ni kuhudumia siasa za Marekani

Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah, imesema kwamba lengo kuu la vikwazo vilivyowekwa na nchi za Kiarabu dhidi ya Syria ni kuhudumia maslahi na siasa za Marekani katika eneo nyeti la Mashariki ya Kati.

Imesisitiza kwamba vikwazo hivyo ni hatari kubwa kwa taifa na serikali ya Syria. Taarifa ya Hizbullah imesema kwamba hatua hiyo iliyochukuliwa na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu inakwenda kinyume na maazimio yake yenyewe yanayosisitiza umuhimu wa kuimarishwa ushirikiano kati ya nchi za Kiarabu. Imesema vikwazo dhidi ya nchi ndugu ya Syria ni aibu kubwa kwa ulimwengu wa Kiarabu na kutahadharisha dhidi ya kufanywa jumuiya hiyo kuwa chombo cha kudhamini maslahi ya Marekani katika nchi za Kiarabu.
Hizbullah imezihutubu nchi wanachama wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na kuzifahamisha kwamba vikwazo dhidi ya Syria ni dhulma kubwa kwa taifa na serikali ya nchi hiyo na kwamba havina faida nyingine yoyote ghairi ya kulinda na kutetea maslahi ya Wamagharibi na hasa Marekani katika Mashariki ya Kati. 907630
captcha