IQNA

14:59 - December 01, 2011
Habari ID: 2232470

Mashia na Masunni Lebanon wajadili, 'Imam Hussein AS na Mwamko wa Kiislamu

Kwa munasaba wa Mwezi wa Muharram, kikao cha 'Imam Hussein AS na Mwamko wa Kiislamu' kimeandaliwa Novemba 29 mjini Beirut Lebanon kwa himaya ya Jumuiya ya Maulamaa Waislamu.

Kwa mujibu wa tovuti ya Al Intiqad, kikao hicho kimehudhuriwa na Maulamaa wa Kishia na Kisunni nchini Lebanon.
Kati ya waliohutubu katika hafla hiyo ni Sheikh Ibrahim Amin Al Seyyed Mkuu wa Idara ya Kisiasa ya Hizbullah na Sheikh Maher Hamud, Imamu wa Msikiti wa Quds katika eneo la Saida Lebanon na Sheikh Mohammad Amru mwanachama wa jumuiya hiyo.
Hafla hiyo imeandaliwa kwa mnasaba wa siku hizi za maombolezo ya kuuawa shahidi mjukuu wa Mtume SAW, Imam Hussein AS akiwa na wafuasi wake 72 katika huko Karbala. Kongamano ambalo ni dhihirisho la umoja wa Kiislamu limefanyika katika Ukumbi wa Jumuiya ya Maulamaa Waislamu mjini Beirut.
908328
captcha