IQNA

8:07 - December 19, 2011
Habari ID: 2240987

Wanazuoni wa al-Azhar wataka kulipizwa kisasi dhidi ya wauaji wa katibu wa Dar al-Ifta

Umati mkubwa wa wanazuoni na wanachuo wa chuo cha kidini cha al-Azhar Jumamosi iliyopita walifanya maandamano makubwa katika uwanja wa Chuo hicho wakilaani vikali mauaji yaliyofanywa dhidi ya Katibu wa Dar al-Ifta na kutaka kisasi kilipizwe dhidi ya wahusika wa mauaji hayo.

Kwa mujibu wa gazeti la Yaum as-Sabi' wanazuoni, wanachuo na vijana wanamapinduzi wa Misri walishiriki kwa wingi kwenye maandamano hayo na kutoa nara za kutaka wahusika wa mauaji hayo wafikishwe mahakamani na kisasi kutolewa dhidi yao kutokana na hatua yao ya kumuua Sheikh Imad Iffat, Katibu wa Dar al-Ifta pamoja na watu wengine waliouawa mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu wa Misri.
Sheikh Ali Jumua, Mufti wa Misri pia alishiriki katika maandamano na mazishi hayo ya Sheikh Imad Iffat. Sheikh huyo aliuawa kwa njia ya kutatanisha alipokuwa akishiriki katika mkusanyiko wa Wamisri waliokusanyika mbele ya ofisi ya Waziri Mkuu kulalamikia siasa za wanajeshi wanaoongoza nchi hiyo.
Wamisri wamekuwa wakifanya mgomo mbele ya ofisi hiyo kwa muda wa wiki mbili sasa wakitaka Baraza la Wanajeshi livunjwe na wanapinga serikali mpya ya nchi hiyo inayoongozwa na Waziri Mkuu Kamal al-Janzuri. 917857
captcha