IQNA

Maulidi ya Mtume (saw) kufanyika kitaifa Ufaransa

10:23 - January 29, 2012
Habari ID: 2263892
Mkutano wa kitaifa wa "Maulidi Mwaka 2012" utafanyika nchini Ufaransa tarehe 11 Februari kwa mnasaba wa kuadhimisha siku ya kuzaliwa mbora wa viumbe, Mtume Muhammad bin Abdullah (saw).
Mkutano huo utafanyika kwa hima ya Kituo cha Kiislamu cha mji wa Strasbourg ukihudhuriwa na maulamaa, wasomi na wanafikra na Waislamu wa Ufaransa.
Miongoni mwa ratiba za mkutano huo ni pamoja na programu za kasida za kundi la Asala, vikao vilivyopewa jina la "Mtume wa Uislamu, Nembo ya Fikra Huru", tungo za kumsifu Mtume, hotuba za maulamaa mashuhuri wa Kiislamu na maonyesho ya vitabu vinavyohusu sira na maisha ya Mtume.
Sehemu nyingine ya mkutano huo itahusu mashindano ya watoto na vijana itakayokuwa na maudhui ya 'Mtume Muhammad (saw) katika Mtazamo wa Watoto'. 941608

captcha