IQNA

Semina ya Sauti za Qur'ani kufanyika Chuo Kikuu cha Columbia

20:14 - February 01, 2012
Habari ID: 2266851
Semina iliyopewa jina la "Sauti za Qur'ani Tukufu, Kutafuta Rehma Ndani ya Qur'ani" imepangwa kufanyika tarehe 14 Februari katika Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani.
Tovuti ya Columbiamsa imeripoti kuwa, semina hiyo ni sehemu ya mpango wa Wiki ya Ujue Uislamu inayofanywa kwa hima ya Jumuiya ya Kiislamu ya Chuo Kikuu cha Columbia kuanzia tarehe 9 hadi 19 Februari.
Semina hiyo itachunguza sauti, lahani, mbinu za kijadi za kiraa ya Qur'ani na sifa makhsusi za kilugha za Qur'ani. Vilevile itachunguza ujumbe mkubwa ulioko kwenye kisa cha Nabii Mussa (as) ndani ya kitabu cha Qur'ani Tukufu.
Ratiba nyingine za semina hiyo ni pamoja na 'rangi za Kiislamu', 'sira ya Mtume (saw)', 'jirani Muislamu' na 'swala ya Ijumaa.
Wiki ya Ujue Uislamu inafanyika kwa shabaha ya kuwaelimisha wanachuo na wananchi wa Marekani na kuondoa taswira mbaya iliyoenezwa katika jamii kuhusu dini hiyo tukufu. 945333



captcha