IQNA

Kongamano la pili la Waislamu Marekani kufanyika mwaka huu

14:59 - March 11, 2012
Habari ID: 2289739
Kongamano la pili la Waislamu Nchini Marekani limepangwa kufanyika tarehe 22 na 23 Septemba mwaka huu katika Chuo Kikuu cha DePaul katika mji wa Chicago.
Kongamano hilo litakalokuwa na maudhui ya: "2030, Uislamu Nchini Marekani, Kizazi Kipya" utasimamiwa na Baraza la Waislamu Marekani.
Mada kuu zitakazojadiliwa na kuchunguza katika kongamano hilo ni utambulisho wa Waislamu, maeneo yao, haki zao za kiraia na elimu kwa Waislamu hadi maka 2030.
Masuala mengine yatayojadiliwa ni takwimu kuhusu idadi ya Waislamu nchini Marekani, kiwango cha kushirikishwa kwao katika masuala ya jamii, umuhimu wa mbari ya Muislamu, kiwango cha kushikamana Waislamu na misingi ya dini yao na maeneo ya jamii za Kiislamu hadi mwaka 2030. 969076



captcha