IQNA

Hali ya Waislamu wenye asili ya Afrika nchini Marekani kuchunguzwa

17:16 - April 07, 2012
Habari ID: 2299467
Hali ya Waislamu wenye asili ya Afrika inachunguzwa leo na kesho Jumapili katika kituo cha Utafiti wa Kiafrika-Kimarekani katika Chuo Kikuu cha Harvard nchini Marekani.
Tovuti ya "islamicstudies.harvard" imeripoti kuwa kongamano hilo linasimamiwa na Chuo Kikuu cha Harvard kwa shabaha ya kuchunguza hali na uzoefu wa Waislamu wenye asili ya Afrika wa Marekani nchini humo.
Masuala mengine yanayochunguzwa ni pamoja na matatizo ya Waislamu hao, hali ya wanawake Waislamu wenye asili ya Afrika raia wa Marekani, jamii za Kiafrika- Kimarekani zinazofuata madhehebu ya Shia, utamaduni wa Kiafrika na Kimarekani katika mtazamo wa Uislamu, kigezo kipya cha uongozi wa jamii za Kiislamu na uongozi wa Kiislamu katika jamii za Kiafrika-Kimarekani.
Kongamano hilo litakamilisha kazi zake kesho. 980149


captcha