Ripota wa IQNA huko kusini magharibi mwa Asia Qamar Alim amesema kuwa Taasisi ya Qur'ani ya Lucknow imetangaza kuwa semina hiyo itachunguza wajibu wa wanawake Waislamu katika kuanzisha jamii ya Kiqur'ani na kutoa malezi sahihi kwa mujibu wa mafundisho ya kitabu hicho kitakatifu na Suna za Mtume Muhammad (saw).
Semina hiyo itahutubiwa na Safia Nasim ambaye ni mjumbe wa Kamati Kuu ya Waislamu wa Lucknow, Bi Ghazala Afzur kutoka mji wa Gonda na Bi Rabia ambaye ni miongoni mwa wasimamizi wa semina hiyo.
Wanawake wote wa mji wa Lucknow wamealikwa kushiriki katika semina hiyo kwa shabaha ya kujifunza utamaduni na maarifa ya Qur'ani Tukufu juu ya jinsi ya kulea kizazi bora. 984812