IQNA

Chama cha al Wifaq Bahrain:

Jamii ya kimataifa inapaswa kuwa pamoja na wananchi na si madikteta

21:53 - April 18, 2012
Habari ID: 2307898
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kiislamu ya al Wifaq nchini Bahrain amekemea misimamo ya kindumakuwili ya jamii ya kimataifa kuhusu mapinduzi ya wananchi wa nchi hiyo na kusema kuwa jamii ya kimataifa inapaswa kuwa pamoja na wananchi na si pamoja na madikteta.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya al Wifaq Sheikh Ali Salman amesema kuwa Marekani imekuwa na msimamo dhaifu kuhusu masuala ya Bahrain na imepuuza ukweli wa mambo kuhusu haki za wananchi na uhakika kuhusu mambo mbalimbali ya nchi hiyo.
Sheikh Ali Salman ameitaka jamii ya kimataifa kuwa pamoja na mataifa na kujiweka mbali na madikteta na kusisitiza kuwa jumuiya hiyo itaendeleza uhusiano wake na nchi za Kiarabu na katika uga wa kimataifa kwa ajili ya kutangaza mitazamo ya wapinzani wa Bahrain.
Amesema kuwa jumuiya hiyo itaendelea kuunga mkono maandamano ya amani wa wananchi kwani utawala wa kifalme wa Aal Khalifa unataka kuziba midomo ya wananchi. Amesisitiza kuwa utawala wa Aal Khalifa unapinga marekebisho na hauko tayari kwa ajili ya mazungumzo ya kweli na kambi ya upinzani. 988483







captcha