IQNA

Jarida jipya la ISESCO lachapishwa

16:33 - May 17, 2012
Habari ID: 2328018
Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ISESCO limechapisha tolea la 13 la jarida lake la utafiti wa kisayansi.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA jarida hilo ambalo limetayarisha na Taaisi ya Ustawi wa Utafiti wa Kisayansi katika ISESCO linajumuisha makala 11 za kisayansi ambazo zimeandikwa na wasomo kutoka Mali, Sudan, Malaysia, Iran, Tunisia, Algeria, India na Bangladesh.
Makala hizo zinahusu masuala kama vile utumizi bora wa nishati katika sekta ya kilimo, uboreshaji ardhi za kilimo, viwango bora katika uzalishaji madawa n.k.
Jarida hilo huchapishwa kila mwaka mara mbili kwa lugha ya Kiingereza ambapo wanasayanis kutoka nchi wanachama hupewa fursa ya kuwasilisha makala kuhusua masuala mbali mbali ya kisayansi. Jarida hilo pia linapatikana kwa njia ya kieletroniki kupitia anuania ifuatayo: www.icpsr.org.ma
1009664
captcha