Kwa mujibu wa tovuti ya OIC kikao hicho ambacho kinadhaminiwa na serikali ya Doha kitafanyika chini ya kauli mbiu ya ' Sauti Mpya, Peo Mpya.' Msemaji wa Ikmal Deen Ihsanoghlu, Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu OIC anatazamiwa kufungua kikao hicho hapo kesho Jumanne. Viongozi na wawakilishi wa nchi tofauti za Kiislamu wanatazamiwa kushiriki kwenye kikao hicho ambacho kitajadili hali mpya ya kisiasa katika nchi za Kiarabu, mambo yanayotoa msukumo wa maendeleo na mabadiliko ya kiutamaduni ulimwenguni pamoja na masuala mengine muhimu katika ulimwengu wa Kiislamu. 1018353