IQNA

Kongamano la 'Uhusishaji wa Thamani za Kiislamu' lafanyika Pakistan

18:03 - June 05, 2012
Habari ID: 2340620
Kongamao la 'Uhuishaji wa Thamani za Kiislamu na Kidini' lilifanyika siku ya Jumamosi huko katika ziara la Chora Sharif mwanairfani mashuhuri wa Pakistan katika mji wa Sialkot katika jumbo la Punjab nchini humo.
Wasomi na wanafikra mashuhuri wa Pakistan walishiriki kwenye kongamano hilo lilioanza saa nne mchana kwa wakati wa nchi hiyo. Baadhi ya shakhsia waliozungumza katika kongamano hilo walisisitiza juu ya udharura wa kuzingatiwa mafundisho na tahamani za Kiislamu katika jamii hasa katika kipindi hiki ambacho maadui wa Uislamu wamekuwa wakitekeleza njama hatari kwa ajili ya kuudhoofisha Uislamu. Wamesema nchi za Kiislamu kama vile Pakistan ambazo zinajivunia Uislamu wao zimekuwa zikishambuliwa na kujuhumiwa kwa propaganda za maadui wa Uislamu ili kuzifanya zilegeze misimamo yao na kusalimu amri mbele ya utamaduni wa Magharibi.1023002
captcha