Taarifa ya Wizara hiyo imesema uchunguzi mkali uliofanywa na vitengo kadhaa vya usalama umepelekea kukamatwa watu hao ambao kwa sasa wanashikiliwa huku wakiendelea kusailiwa. Waliokamatwa wamekiri kuwa na mfungamano na utawala haramu wa Israel.
Mostafa Ahmadi Roshan, mwanasayansi wa nyuklia wa hapa Iran aliuawa mwezi Januari mwaka huu baada ya bomu kutegwa kwenye gari lake.
Novemba mwaka 2010 mtaalamu mwingine wa nyuklia hapa nchini, Prof. Majid Shahriari aliuawa baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.
1030240