IQNA

Ayatullah Jannati: Iran haitapuuza haki yake kufaidika na teknolojia ya nyuklia

14:43 - June 16, 2012
Habari ID: 2347718
Khatibu wa muda wa Sala ya Ijumaa hapa mjini Tehran amesema leo kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kamwe haitofumbia macho haki yake ya kustafidi na teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani.
Ayatullah Ahmad Jannati amekumbusha kwamba Iran imepitia kipindi kigumu cha uchokozi kutoka kwa dikteta wa zamani wa Iraq, Saddam Hussein aliyekuwa akiungwa mkono na Wamagharibi na pia vikwazo vya zaidi ya miaka 30 vya Marekani na kwa mantiki hiyo nchi hii haiwezi tena kutishwa wala kubabaishwa na yeyote.
Akizungumzia mazungumzo yajayo kati ya Iran na kundi la 5+1, Ayatullah Jannati amesema Iran itaingia kwenye mazungumzo hayo na mtazamo wa ushirikiano na wala sio kuwapigia magoti Wamagharibi. Amesisitiza kuwa takwa la Iran ni kuheshimiwa haki yake ya kurutubisha urani kwa malengo ya amani kwa mujibu wa sheria za Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA. Mazungumzo hayo yanatarajiwa kufanyika Juni 18 na 19 mjini Moscow, Russia.
1030379
captcha