IQNA

Serikali ya Marekani, mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu

19:29 - June 20, 2012
Habari ID: 2351014
Sarah Flanders ambaye ni miongoni mwa wakurugenzi wa kituo cha kimataifa cha kupinga vita na ubepari cha The International Action Center (IAC) anaamini kwamba Marekani ndiyo mkiukaji mkubwa wa haki za binadamu duniani.
Kanali ya televisheni ya Press imemnukuu Sarah Flanders akisema kuwa hii leo Marekani ndiye mkiukaji mkuu wa haki za binadamu duniani ndani ya nchi na katika medani ya kimataifa.
Kituo cha The International Action Center (IAC) kinakusanya pamoja wanaharakati wanaopinga vita na siasa za kibepari za Marekani.
Flanders amesema kuwa harakati ya kuteka Wall Street ni mfano wa yale yanayotendeke mara kwa mara nchini Marekani.
Amesema kutiwa mbaroni kwa wingi watu wasiokuwa na hatia, kutolewa taswira isiyokuwa sahihi kuhusu vyombo vya habari na kuwatambua vijana wanaopigania haki zao kuwa ni wahalifu ni mifano ya wazi ya ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu unaofanywa na serikali ya Marekani. 1034438




captcha