IQNA

Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya Najaf:

Utawala wa Aal Saud unashirikiana na Wazayuni

9:01 - July 01, 2012
Habari ID: 2357826
Imam wa Sala ya Ijumaa katika mji mtakatifu wa Najaf nchini Iraq amesema kuwa utawala wa Aal Saud huko Saudi Arabia ni utawala fasidi na ulioanzishwa kwa msingi wa kushirikiana na Israel na kuendeshwa kwa msingi wa ukabila.
Sayyid Sadruddin al Qubanchi aliyekuwa akihutubia katika Husainiya ya Fatimiyya mjini Najaf amesema kuwa utawala uliopotoka wa Saudia unapaswa kubadilika katika zama hizi za mwamko wa mataifa mbalimbali.
Ameongeza kuwa Mashia na Masuni wa Saudia wamechoshwa na utawala wa kiimla wa Riyadh na wanahitaji msaada.
Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, hatibu wa Sala ya Ijumaa ya Najaf amegusia mgogoro wa sasa wa Syria na kusema kunashuhudia misimamo ya kindumakuwili dhidi ya nchi hiyo na makundi ya upinzani yanasaidiwa na nchi za kigeni.
Amesema kuwa wapinzani wa serikali ya Syria wanasaidiwa ya nchi za nje huku wananchi wa Bahrain wakiendelea kunyanyaswa na utawala wa nchi hiyo na kupuuzwa na jumuiya za kimataifa. Amesema jeshi la Ngao ya Kisiwa ambalo Saudia ni mwanachama wake pia limepelekwa Bahrain kuwakandamiza wanamapinduzi wanaopigania haki zao za kiraia. 1040943

captcha