IQNA

Muadhini wa Msikiti wa Mtume (saw) mjini Madina aaga dunia

13:02 - July 09, 2012
Habari ID: 2364200
Sheikh Hussein bin Abdullah Rajab, muadhini wa Msikiti wa Mtume (saw) mjini Madina aliaga dunia Ijumaa iliyopita akiwa na umri wa miaka 85.
Kwa mujibu wa gazeti la al-Watan linalochapishwa nchini Saudia Sheikh Abdallah Rajab amekuwa akiadhini kwenye msikiti huo kwa zaidi ya miaka 50. Alizikwa siku ya Jumamosi katika makaburi ya Baqii baada ya kuswaliwa swala ya maiti katika Msikiti wa Mtume (saw).
Sheikh Abdullah Rajab alizaliwa mwaka 1348 Hijiria katika mji wa Madina na kupata masomo yake katika mji huohuo. Aliteuliwa kuwa mwadhini rasmi wa msikiti huo mwaka 1385.
Kabla ya kuwekwa mitambo ya kisasa ya sauti kwenye msikiti huo, Abdullah Rajab alikuwa akiadhini kupitia minara ya msikiti huo lakini baada ya kupatwa na maradhi adhana yake imekuwa ikisikika nyakati za asubuhi tu. 1047449
captcha