IQNA

Mashindano ya Qur'ani Tukufu kuonyeshwa katika televisheni ya Jordan

15:41 - July 18, 2012
Habari ID: 2371764
Vipindi vilivyosajiliwa awali vya duru ya pili ya mashindano ya kiraa ya Qur'ani Tukufu yaliyopewa jina la Zawadi ya Msomaji wa Jordan vitarushwa hewani kupitia televisheni ya taifa na Idhaa ya Qur'ani ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa gazeti la nchi hiyo la as-Sabil, Gassan az-Zuweidi mkurugenzi mratibu wa zawadi hiyo amesema mashindano hayo yaliyowashirikisha wasomaji bora wa Qur'ani kutoka mikoa yote ya Jordan yatapeperushwa hewani kupitia vyombo vilivyotajwa vya habari katika mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Amesema lengo la kuandaliwa mashindano hayo ni kujaribu kutafuta watu walio na vipawa vya usomaji Qur'ani miongoni mwa Wajordan ambapo 100 kati ya hao tayari wamefanikiwa kuingia katika duru ya mwisho ya mashindano hayo ambayo itafanyika mwishoni mwa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Amesema mshindi wa kwanza atazawadiwa gari. Waandaaji wa mashindano hayo wamesema lengo jingine ni kuhudumia Qur'ani na kuwaandaa wasomaji wa nchi hiyo waweze kushiriki katika mashindano ya kitaifa na kimataifa ya Qur'ani Tukufu. 1055199
captcha