Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukaribisha Madhehebu ya Kiislamu (WFPIST), Hujjatul-Islam Hamid Shahriari, alizungumza kabla ya khutba ya Ijumaa wiki hii mjini Tehran, na kusisitiza kuwa umoja wa Kiislamu katika ngazi ya kitaifa, kikanda na kimataifa ni lazima uimarishwe ili kukabiliana na ubabe wa upande mmoja wa Marekani.
Aliwapongeza waumini kwa kuwadia kwa Wiki ya Umoja wa Kiislamu, akieleza kuwa WFPIST imekuwa ikihifadhi fikra hii ya thamani kwa miaka 38 kupitia Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu, na imefikisha ujumbe wa mshikamano kwa ulimwengu mzima.
Mwaka huu, kwa kuadhimisha miaka 1500 tangu kuzaliwa kwa Mtume Mtukufu Muhammad (SAW), Mkutano wa 39 wa Umoja wa Kiislamu wenye kaulimbiu "Mtume wa Rehema" utafanyika kuanzia Jumamosi hadi mwisho wa wiki.
Nguzo za Umoja wa Kiislamu
Katika kufafanua dhana ya umoja, Hujjatul-Islam Shahriari alieleza kuwa kuna angalau thamani tatu za Kiislamu zinazounda msingi wa mshikamano:
Palestina: Alama ya Mshikamano wa Dunia
Hujjatul-Islam Shahriari aliongeza kuwa Palestina imekuwa alama ya mshikamano kwa sababu nguzo hizi tatu yaani heshima, haki na usalama, zimekiukwa vibaya. "Hata wasiokuwa Waislamu wanaitetea Palestina kwa sababu wanatambua thamani ya utu, haki na usalama."
"Sifa hizi tatu—heshima ya binadamu, haki, na usalama—zinaeleweka kwa kila mwanadamu, na ndiyo maana hata wasiokuwa Waislamu wanaitetea Palestina. Kutetea heshima ya binadamu, haki, na usalama si jambo la Waislamu pekee; kwa hivyo, katika mitaa ya nchi za Magharibi, watu hujitokeza kwa wingi kuunga mkono Palestina na kulaani utawala wa Israel."
Ujumbe wa Qur’an na Wito kwa Waislamu
Aidha msomu hiyo alinukuu aya tukufu ya Qur'ani isemayo: “Shikamaneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote, wala msifarakane.” (Surah Al-Imran, aya ya 103) Akasema kuwa kila kitu kinachosababisha mgawanyiko ni haramu. Waislamu wa Sunni na Shia wanapaswa kusimama pamoja dhidi ya maadui kwa kushikamana na kamba ya Mwenyezi Mungu.
Ushirikiano wa Kikanda
Kuhusu umuhimu wa umoja wa Kiislamu baina ya nchi za Kiisalmu katika eneo la Asia Magharibi, alisema: "Lazima tuzingatie kwa makini nchi jirani na zile za Kiislamu; nchi kama Pakistan, Uturuki, Saudi Arabia, na Misri ni muhimu sana. Tunapaswa kuimarisha hisia za udugu na nchi hizi. Hasa Misri, ambayo wakati mmoja iliungana na nchi 20 za Kiislamu kulaani shambulio la (utawala wa Israeli) dhidi ya Iran (mnamo Juni). Hizi ndizo uwezo wa ulimwengu wa Kiislamu, na taifa lililoungana lazima litegemee kamba ya Mwenyezi Mungu ili kuzuia uingiliaji wa adui."
Wiki ya Umoja wa Kiislamu
Wiki hii huadhimishwa kati ya tarehe 12 na 17 ya mwezi wa Rabi al-Awwal, tarehe ambazo Sunni na Shia huamini kuwa ni siku ya kuzaliwa kwa Mtume Muhammad (SAW). Wiki hii ilitangazwa na Imam Khomeini katika miaka ya 1980 kama ishara ya kuleta umoja miongoni mwa Waislamu.
3494485