IQNA

Mashindano ya makala na usomaji Qur'ani katika mwezi wa Ramadhani nchini Nigeria

16:34 - July 29, 2012
Habari ID: 2380101
Serikali ya Nigeria ina lengo la kuandaa mashindano ya uandishi makala na usomaji wa Qur'ani Tukufu maalumu kwa wanafunzi katika jimbo la Ugon katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Rashida Salimu, mratibu wa mashindano hayo amesema kwamba lengo la kuandaliwa mashindano hayo ni kunyanyua kiwango cha ufahamu wa wanafunzi kuhusiana na Uislamu na fadhila za mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Amefafanua kwamba jambo hilo litawawezesha wanafunzi kutafiti kuhusu jambo hilo na hivyo kuimarisha viwango vyao vya utambuzi wa mambo.
Amesema zawadi zitatolewa mwishoni mwa mwezi wa Ramadhani kwa wanafunzi watakaofanya vyema katika mashindano hayo.
Sehemu ya kwanza ya mashindano hayo ilifanyika Jumatano iliyopita na sehemu ya pili ambayo itahusiana na usomaji Qur'ani imepangwa kufanyika siku ya Jumanne ijayo. 1063959
captcha