IQNA

Wiki ya Hifdhi ya Qur’ani kufanyika Ubelgiji

16:32 - July 29, 2012
Habari ID: 2380145
Wiki ya Hifdhi ya Qur’ani Tukufu itaanza tarehe 1 Agosti nchini Ubelgiji chini ya usimamizi wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (ISESCO).
Wiki hiyo itafanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Masuala ya Kiislamu, Wakfu, Ulinganiaji na Mwongozo ya Saudi Arabia na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu ya Ubelgiji.
Miongoni mwa malengo ya shughuli za wiki hiyo ni kukidhi mahitaji ya Waislamu wanaoishi nje ya ulimwengu wa Kiislamu katika uwanja wa hifdhi ya Qur’ani, elimu ya Qur’ani, kulinda utambulisho wa Kiislamu katika nchi za Magharibi na kuimarisha thahamani za Kiislamu. 1064124


captcha