IQNA

Kikao cha ‘Tafsiri ya Qur’ani’ chafanyika Nigeria

16:57 - July 31, 2012
Habari ID: 2381428
Kikao cha ‘Tafsiri ya Qur’ani Tukufu’ kimefanyika Julai 28 chini ya usimamizi wa Taasisi ya Ahul Bayt AS katka Msikiti wa Jamia Lagos.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, kikao hicho kilihudhuriwa na Sheikh Zaghloul, Sayyed Baqir, Sayyid Javadi mkuu wa idara ya utamauni Iran nchini Nigeria.
Akihutubia kikao hicho, Sayyid Javadi, amezungumzia fadhila za Ahlul Bayt AS pamoja na utakasaji wa nafsi katika mwezi huu mtukufu pamoja na umuhimu wa dua kwa mtazamo wa Ahlul Bayt AS.
Huku akiashiria namna Qur’ani Tukufu ilivyosisitiza juu ya suala la udugu, amesema umoja ni hitajio la dharura katika jamii za Kiislamu.
1065765
captcha