IQNA

Mashindano ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani yaanza Guinea Conakry

18:01 - July 31, 2012
Habari ID: 2382312
Mashindano ya kitaifa ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani Tukufu yamezinduliwa rasmi katika mji mkuu wa Guinea Conakry.
Mashindano hayo ambayo ni ya 31 ya hifdhi na kiraa ya Qur'ani yalianza Jumapili iliyopita yakiwashirikisha makarii na mahafidhi 179 kutoka miji mbalimbali ya Guinea.
Mkurugenzi taifa wa Jumuiya ya Masuala ya Kiislamu ya Guinea Conakry Bala Diane alisema katika sherehe ya kufungua mashindano hayo kwamba anatarajia kuwa mashindano hayo yatakuwa hatua muhimu ya kuwahamasisha wanafunzi wa shule na vyuo vikuu vya nchi hiyo kutilia maanani utamaduni wa Qur'ani Tukufu.
Mashindano hayo yatamalizika tarehe Agosti katika sherehe itakayohudhuriwa na viongozi wa kiserikali na kidini. 1067212
captcha