Baada ya kufunguliwa maonyesho hayo kwa kiraa ya msomaji wa kimataifa wa Iran Hassan Ridhaiyan, mkuu wa Maktaba ya Taifa ya Tunisia aliishukuru Iran kwa ushirikiano mzuri katika kuanzisha maonyesho ya nakala za Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono.
Amesema kuwa nakala 37 za Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono ambazo baadhi yao ziliandikwa katika karne ya 2 na 4 zinaonyeshwa kwenye maonyesho hayo. Amesema 21 kati ya nakala hizo zimetoka katika Maktaba ya Taifa ya Iran na 16 zilitoka kwenye Maktaba ya Taifa ya Tunisia.
Mwambata wa utamaduni wa Iran nchini Tunisia Sadiq Ramadhani pia amesema kuwa jumba la makumbusho la Maktaba ya Taifa ya Iran iko tayari kupanua zaidi ushirikiano wa kiutamaduni na taasisi husika hususan Maktaba Kuu ya Tunsia. 1070154