IQNA

Bunge la Misri lapinga kuchapishwa Qur'ani yenye juzuu 28

13:56 - August 12, 2012
Habari ID: 2390999
Mwakishi mmoja wa Bunge la Misri ametangaza kuwa nakala elfu 40 za Qur'ani Tukufu zimechapishwa nchini humo zikiwa na juzuu 28 tu za Qur'ani Tukufu.
Taarifa iliyotolewa na mbunge huyo imesema nakala hizo za Qur'ani ina juzuu 28 tu na ina kasoro ya juzuu mbili za Qur'ani Tukufu.
Amesisitiza kuwa nakala hizo elfu 40 za Qur'ani zimechapishwa katika kiwanda cha uchapishaji cha al Tawfiqiyya chini ya usimamizi wa Sheikh Ahmad al Nasrawi ambaye ni miongoni ma mashekhe wa chuo cha al Azhar. Ameongeza kuwa makosa hayo ni makubwa kiasi kwamba hayaweza kufumbiwa macho na ni ya makusudi.
Wakati huo huo Spika wa Bunge la Misri Ahmad Fahmi amewasilisha suala hilo kwa Sheikh wa al Azhar Ahmad al Tayyib na Kamati ya Fatuwa ya Misri na kuwataka kufuatilia suala hilo kwa bidii. 1074961
captcha