IQNA

Kitengo cha kimataifa katika maonyesho ya kimataifa ya Qur'ani ya Tehran chafungwa

19:07 - August 12, 2012
Habari ID: 2391130
Kitengo cha Kimataifa katika Maonyesho ya Kimataifa ya 20 ya Qur'ani Tukufu mjini Tehran kimefungwa rasmi leo Jumapili katika sherehe maalumu.
Sherehe hizo zilizofanyika leo saa 12 jioni kwa wakati wa Tehran zimehudhuriwa na viongozi wa masuala ya kiutamaduni na Kiislamu nchini.
Kitengo hicho cha kimataifa kilifunguliwa Jumatatu Julai 30 ambapo wasanii, wasomi, wanazuoni, wataalamu na watafiti wa masuala ya Kiislamu na Qur'ani Tukufu kutoka nchi mbalimbali za dunia wamekua wakikitembelea na kunufaika na masuala tofauti yanayoonyeshwa na kuendeshwa katika kibanda hicho.
Kitengo hicho kilichoendesha shughuli zake kwa muda wa siku 10 kimewezesha washiriki wa maonyesho hayo kuwasilisha vitabu, mabango na kazi tofauti za mikono zinazohusiana na Qur'ani Tukufu. 1076673
captcha