IQNA

Wafanyakazi wa Msikiti Mkuu wa Makka wapewa mafunzo ya Huduma ya Kwanza

17:51 - September 12, 2025
Habari ID: 3481218
IQNA – Warsha ya mafunzo kuhusu stadi za msingi za huduma ya kwanza imefanyika kwa wafanyakazi wa Msikiti Mkuu, Masjid Al Haram, ulioko katika mji mtukufu wa Makka.

Mamlaka ya Hilali Nyekundu ya Saudi katika mkoa wa Makka imemaliza rasmi warsha hiyo, ambayo imewanufaisha zaidi ya washiriki 3,860, kwa mujibu wa Shirika la Habari la Saudi (SPA).

Mafunzo hayo yalijumuisha vipindi vya nadharia na vitendo kuhusu jinsi ya kukabiliana na hali za dharura za kawaida kama vile kuzimia, kushindwa kupumua, kutokwa na damu, na majeraha madogo.

Washiriki pia walipata mafunzo ya moja kwa moja kuhusu uokoaji wa moyo na mapafu (CPR) pamoja na matumizi ya kifaa cha kielektroniki cha kuchochea moyo (AED).

Mamlaka hiyo ilihakikisha kuwa programu hiyo ilitolewa kwa lugha za Kiarabu na Kiurdu, ili kufikisha maarifa muhimu kwa wafanyakazi wa mataifa mbalimbali na kuongeza uwezo wao wa kukabiliana na dharura kwa ufanisi.

3494565

Msikiti Mkuu wa Makka hupokea mamilioni ya mahujaji wa Hajj na Umrah kutoka kila pembe ya dunia kila mwaka.

Kishikizo: makka huduma umrah hija
captcha