IQNA

Mahafali ya Qur'ani Tukufu yanafanyika kila siku katika Haram ya Abulfadh Abbas (as).

13:39 - August 14, 2012
Habari ID: 2392787
Kitengo cha Utamaduni cha Haram ya Abulfadhil Abbas (as) katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq kimeadaa mahafali ya kila siku ya usomaji Qur'ani katika haramu hiyo kutokana na idadi kubwa ya wafanyaziara wa Kiirani wanaozuru haram hiyo na ile iliyo karibu ya Imam Hussein (as).
Kitengo hicho kimetangaza kuwa mahafali hiyo ya kufarijika na Qur'ani huanza mara tu baada ya kusimamishwa swala za Adhuhuri na Alasiri.
Ripoti hiyo inasema kuwa nukta ya kuvutia katika mahafali hiyo ni kuona watu wa mataifa mbalimbali wakikusanyika pamoja kwa ajili ya kusoma kitabu hicho cha wahyi wa Mwenyezi Mungu.
Inasema jambo jingine la kuvutia ni kuona idadi kubwa ya wafanyaziara wa Iran wakishiriki kwa hamu kubwa katika mahafali hiyo. 1077903
captcha