IQNA

Mamilioni watakiwa kuhitimisha Qur'ani katika Medani ya Tahrir

16:03 - August 15, 2012
Habari ID: 2393966
Chama cha Uhuru na Uadilifu cha Harakati ya Ikhwanul Muslimin nchini Misri kimewataka mamilioni ya wananchi kuhudhuria katika Medani ya Tahrir mjini Cairo hapo kesho kwa ajili ya kuhitimisha Qur'ani Tukufu.
Chama hicho kimewataka Wamisri kuhudhuria kwa wingi katika mahfali hiyo ya Qur'ani na kutangaza uungaji mkono wako kwa Rais Muhammad Mursi wa nchi hiyo.
Katibu Mkuu wa Harakati ya Ikhwanul Muslimin amesema kuwa harakati hiyo na vyama vingine vya kitaifa na kimapinduzi vitashiriki katika mjumuiko huo wa mamilioni ya watu kwa ajili ya kuhitimisha Qur'ani Tukufu ambapo pia vitatangaza uungaji mkono wao kwa maamuzi yaliyochukuliwa na Rais Mursi. 1079459

captcha