Sherehe hiyo ilifanyika kwa lengo la kuwashukuru waandaaji na washindi wa mashindano hayo yaliyopewa jina la Taj al-Qur'ani.
Rais Bourteflika aliwapa zawadi washindi wa kwanza hadi tatu wa mashindano hayo ya kimataifa ambao walikuwa ni kutoka katika nchi za Libya, Bangladesh na Chad kwa utaratibu. Vilevile aliwashukuru waandaaji, wasimamizi na kamati ya waamuzi wa mashindano hayo ya kimataifa.
Mbali na ujumbe wa serikali, mabalozi wa nchi kadhaa za Kiislamu pia walishiriki katika sherehe hiyo.
Wawakilishi wa nchi 50 walishiriki katika mashindano hayo yaliyoanza tarehe 8 Agosti na kukamilika jana Jumanne mjini Algiers.1079364