IQNA

Maonyesho ya Qur'ani ya kale Istanbul

20:44 - August 28, 2012
Habari ID: 2400918
Nakala za kale na mpya za Qur'ani Tukufu zitaonyeshwa katika maonyesho ya kitamaduni na Kiislamu 2012 katika mji wa Istanbul huko Uturuki.
Maonyesho hayo yanafanyika kwa ushirikiano wa Kituo cha Masuala ya Kidini cha China na Jumuiya ya Masuala ya Kidini ya Uturuki kwa mnasaba wa kuadhimisha mwaka wa kiutamaduni wa nchi hizo mbili.
Maonyesho hayo yatajumuisha nakala za kale za Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono, matunda ya kiutamaduni na Kiislamu ya Waislamu wa China na maonyesho ya kaligrafia.
Sehemu moja ya maonyesho hayo itahusu kazi za wasanii wa Kiislamu wa China na athari za kihistoria na kiutamaduni za miaka 300 iliyopita. 1086853
captcha