IQNA

Makarii wa Iran waongoza mashindano ya kimataifa ya Qur’ani ya wanafunzi wa vyuo vikuu

23:55 - September 15, 2012
Habari ID: 2412081
Awamu ya mwisho ya mashindano ya kimataifa ya Qur’ani ya wanafunzi Waislamu wa vyuo vikuu ilimalizika jana katika mji wa Tabriz huko kaskazini magharibi mwa Iran. Hafidhi na karii wa Jamhuri ya Kiislamu wameongoza katika mashindano hayo.
Fainali ya mashindano hayo ilifunguliwa kwa kiraa ya Ustadh Abdul Fattah al Taruti ambaye alikuwa miongoni mwa majaji wa mashindnao hayo kutoka Misri.
Sehemu ya hifdhi ya Qur’ani nzima ilishirikisha washindani saba na kiraa ilikuwa na washindani 6.
Katika mashindano ya hifdhi ya Qur’ani nzima Abu Dharr Karami wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameshika nafasi ya kwanza baada ya mchuano mkali uliokuwa na mahafidhi kutoka nchi za Mauritania, Misri, Indonesia, Tajikistan, Uganda na Qatar.
Katika upande wa kiraa ya Qur’ani, Majiid Faqihi wa Jamhuri ya Kiislamu ameshika nafasi ya kwanza na kuwaacha nyuma makarii kutoka Lebanon, Kuwait, Ujerumani, Afghanistan na Bahrain.
Sherehe za kuhitimisha duru ya 4 ya mashindano ya Kimataifa ya Qur’ani Tukufu ya wanafunzi Waislamu wa vyuo vikuu zilianza mapema jana. Mashindano hayo yamewashirikisha wawakilishi wa nchi 52. 1098364

captcha