Mahakama ya Russia imeeleza kwamba, filamu hiyo haipaswi kuonyeshwa nchini humo, kwani inamvunjia heshima Mtume SAW, na inapingwa na Waislamu kote ulimwenguni.
Wakati huohuo, Waislamu nchini Afrika Kusini walifanya maandamano makubwa jana wakilaani vikali utengenezwaji wa filamu hiyo na kusisitiza kwamba kamwe hawatakubali kuona matukufu ya Kiislamu yakidhalilishwa na kuvunjiwa heshima.
Waislamu wa mjini Johannesburg walikusanyika mbele ya Ubalozi mdogo wa Marekani mjini humo, na kupiga nara dhidi ya Marekani. Aidha Waislamu hao wameitaka serikali ya Marekani kuwatia mbaroni wale wote waliohusika katika kutengeneza filamu hiyo inayotusi matukufu ya Kiislamu sanjari na kupigwa marufuku nchini humo.
1109075