IQNA

Programu ya kwanza ya tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya ishara kuzinduliwa Gaza

15:10 - September 30, 2012
Habari ID: 2423028
Waziri wa Elimu ya Juu wa Palestina amesema kuwa programu ya kwanza ya tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya ishara itazinduliwa hivi karibuni.
Usama al Mazini amesema kuwa, wataalamu wa Kipalestina wamefanikiwa kutengeneza programu ya kwanza ya tarjumi ya Qur'ani Tukufu kwa lugha ya ishara itakayotumiwa na viziwi. Ameongeza kuwa kazi hiyo itazinduliwa hivi karibuni.
Programu hiyo ya tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya ishara imetengenezwa kwa usimamizi wa Wizara ya Elimu ya Juu na kwa kushirikiana na Jumuiya ya Mustakbali wa Viziwi na Taasisi ya Nyumba ya Qur'ani.
Programu hiyo inajumuisha CD ya juzuu 30 za Qur'ani Tukufu. 1110290
captcha