IQNA

13:47 - November 15, 2012
Habari ID: 2448837

Iran yalaani kimya cha kimataifa kufuatia ukatili wa Israel huko Ghaza

Iran imekosoa vikali kimya cha jamii ya kimataifa hasa Baraza la Kutetea Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mkabala na jinai za Israel huko Palestina na kusisitiza kuwa, kimya hicho kinaipa kiburi Israel cha kuendelea kuishambulia Gaza.

Katika taarifa, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Ramin Mehmanparast pia amesema kuwa, mashambulizi ya kijeshi ya utawala haramu wa Israel huko Gaza yanayopelekea kuuawa na kujeruhiwa makumi ya wananchi wa Palestina kwa mara nyingine yanathibitisha hatua za kikatili za utawala huo.

Mashambulizi ya Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza yaliyosababisha kuuawa shahidi Wapalestina kadhaa yamelaaniwa na kukabiliwa na radiamali kali ya jamii ya kimataifa.

Rais Muhammad Morsi wa Misri kupitia msemaji wake amelaani jinai hizo na kulitaka Baraza la Usalama kuitisha kikao cha dharura kujadili mashambulizi hiyo. Pia kufutia mashambulizi hayo Misri imemwita nyumbani balozi wake huko Israel.


1137767
captcha