IQNA

Rais mteule wa Nigeria Muhammadu Buhari

Magaidi wa Boko Haram hawana uhusiano na dini

12:47 - April 30, 2015
Habari ID: 3233862
Rais mteule wa Nigeria amesema kuwa, hakuna dini yoyote ile inayounga mkono jinai zinazofanywa na kundi la kitakfiri la Boko Haram.

Muhammadu Buhari amebainisha kwamba, madai ya Boko Haram ya kuzihusisha harakati zake na dini hayana ukweli wowote kwani hakuna itikadi ya dini yoyote ile ambayo inayohalalisha jinai au kuua watoto wa shule. Rais huyo mteule wa Nigeria alimshinda Goodluck Jonathan katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni. Buhari amesisitiza kuwa, Boko Haram ni kundi la kigaidi na kwamba, serikali yake itapambana na kundi hilo kwa mujibu wa mbinu na mikakati ya kukabiliana na magaidi. Muhammadu Buhari amemtuhumu Rais Gooluck Jonathan  anayeondoka kwamba, ameshindwa kukabiliana vilivyo na tishio la usalama linaloikabili nchi hiyo. Buhari amesisitiza kuwa, wakati umefika wa kufanyika mabadiliko na mageuzi makubwa nchini humo.../EM

3214408

captcha