IQNA

Mtoto wa miaka 3 Algeria ahifadhi Qur'ani yote

11:27 - March 10, 2014
Habari ID: 1385230
Abdul-Rahman Farih ndie mtu mwenye umri wa chini zaidi duniani kuhifadhi kilamilifu Qur'ani Tukufu.

Kwa mujibu  wa mwandishi wa Shirika la Kimataifa la Habari za Qur'ani IQNA, tovuti ya www.egypty.com imeripoti kuwa mtoto huyu kutoka Algeria ana umri wa miaka mitatu na amewavutia watu wengi kote duniani kutokana na uwezo wake mkubwa wa kuhifadhi aya zote za Qur'ani na kusoma kutoka moyoni. Aidha ana uwezo mzuri wa kusoma Qur'ani kwa mbinu ya tarteel. Imearifiwa kuwa ameihifadhi Qur'ani kwa kushiriki katika vyuo vya Qur'ani na misikitini. Mtoto huyo Mualgeria alianza kuhifadhi Qur'ani akiwa na umri wa miaka miwili wakati alipoanza kuzungumza na alifanikiwa kuhifadhi Qur'ani yote kwa muda wa mwaka moja.  Kanali ya televisheni ya MBC imerusha hewani ripoti kuhusu mtoto huyo mwerevu na kusema Abdu-Rahman ana kipaji cha kipekee cha kusoma Qur'ani kwa tarteel kwa kuzingatia kanuni zote za usomaji pasina kufanya kosa. Mtoto huyo awali kabisa alihifadhi Surah Al Kahf. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, mama yake mtoto huyo alikuwa akisoma sana Surah Al Kahf wakati akiwa mja mzito  kutokana na kuwa surah hiyo ilikuwa ikimpa utulivu mkubwa wa moyo.
1384655

captcha