Gazeti la Jakarta Post limeandika kuwa Mwanamfalme Charles ambaye yuko katika safari ya siku tano ya kuitembelea Indonesia amesema, hekima na busara ya dini mbalimbali duniani inaweza kusaidia juhudi za kupambana na maadui wa pamoja ikiwa ni pamoja na umaskini na kubakia nyuma kimaendeleo.
Mwanamfalme Charles wa Uingereza anatarajiwa kukutana na Rais Susilo Bambang Yudhoyono wa Indonesia hii leo. Pande hizo mbili zitajadili matatizo yanayowakabili wafuasi wa dini mbalimbali duniani. 314515