IQNA

Maonyesho ya Kimataifa ya Bidhaa Halali nchini Imarati

12:15 - November 13, 2008
Habari ID: 1707790
Maonyesho ya kimataifa ya Bidhaa halali ya mwaka huu wa 2008 yamefunguliwa wiki hii katika kituo cha maonyesho cha Abu Dhabi.
Gazeti la Khalij Times limeandika kuwa lengo la maonyesho hayo yanayowashirikisha wanahakati wa kiuchumi na wawekezaji kutoka vituo vya fedha vya Kiislamu ni kutayarisha uwanja mzuri wa kustawisha bidhaa halali kote duniani.
Katika maonyesho hayo ya siku tatu yanayozishirikisha nchi kadhaa za Kiislamu na zisizokuwa za Kiislamu, kutaonyeshwa baadhi ya vielelezo vya ustawi wa uwekezaji wa Kiislamu. Vilevile vikao vitatu vya kitaalamu kuhusu benki ya Kiislamu vitafanyika kandokando ya maonyesho hayo. 319480
captcha