IQNA

Mfumo wa kwanza wa kuratibu kiumri michezo ya kompyuta ya nchi za Kiislamu

12:59 - December 28, 2008
Habari ID: 1723717
Mfumo wa kwanza wa kuratibu michezo ya kompyuta ya nchi za Kiislamu kwa msingi wa umri wa wanaoicheza michezo hiyo umezinduliwa na Waziri wa Utamaduni na Muongozo wa Kiislamu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Tehran.
Mfumo huo umezinduliwa baada ya michezo hiyo kukaguliwa na kuchunguzwa kwa makini kwa muda wa mwaka mmoja na wataalamu wa vyuo vikuu na vituo vya kidini. Wengine waliochangia katika kuufanikisha mfumo huo ni pamoja na wataalamu wa masuala ya nafsi na elimu jamii.
Sherehe za uzinduzi wa mfumo huo muhimu na wenye athari kubwa katika kulea jamii iliyo salama, zimehudhuriwa na viongozi wa serikali kutoka wizara na idara mbalimbali zinazohusika na masuala ya kijamii na utamaduni pamoja na wasanii mashuhuri wa humu nchini.338726
captcha