IQNA

Hatua ya mwisho ya mashindano ya kitaifa ya hifdhi na kusoma Qur'ani mjini Dubai

9:58 - February 15, 2009
Habari ID: 1744184
Hatua ya mwisho ya mashindano ya pili ya kuhifadhi na kusoma Qur'ani Tukufu ya Zawadi ya Dubai yameanza leo mjini humo na yataendelea hadi tarehe 23 Februari.
Ibrahim Muhammad Bumulihha, mkuu wa kamati inayosimamia mashindano hayo anasema kuwa, mashindano hayo yanafanyika kwa ushirikiano wa taasisi za Kiislamu na mashirika ya vyombo vya habari na magazeti muhimu ya Umoja wa Falme za Kiarabu. Amesema, mashindano hayo yanafanyika katika makundi mawili ya wanaume na wanawake na kwamba yanafanyika kwa uungaji mkono na msaada wa Muhammad bin Rashid Aal Maktum, mtawala wa Dubai na kwa ushirikiano wa Taasisi ya Zawadi ya Qur'ani ya Dubai.
Bumulihha amesema kuwa, kwa kuzingatia ukaribisho mkubwa ambao umeonyeshwa na wapenzi wa Qur'ani kwa mashindano hayo, kamati inayosimamia mashindano hayo imesema kuwa, wasimamizi pia wataandaa mashindano ya kuhifadhi juzuu tatu za Qur'ani maalumu kwa watoto walio na umri wa chini ya miaka kumi. Amesema, nyanja za kusoma na kuhifadhi Qur'ani nzima zimeongezwa katika mashindano ya zawadi hiyo ya Dubai.
Mkuu huyo wa zawadi ya Dubai amemalizia kwa kusema, hatua za mwanzo za mashindano hayo zilifanyika awali katika miji ya Dubai, Abu Dhabi, Sharjah, Ras al-Kheimah, Ajman, Ummu Qawiyain na al-Ain huko Imarati.
Washindani walioshinda katika hatua hiyo ndio waliofanikiwa kushiriki katika hatua hii ya pili na ya mwisho ya mashindano ya Zawadi ya Dubai. 363727
captcha