Katika taarifa hiyo, Bernard Kouchner, Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Ufaransa amelaani vikali hatua hiyo ya makundi ya kigaidi yenye misimamo ya kupindukia mipaka dhidi ya waombolezaji waliokuwa njiani kuelekea Karbala kwa ajili ya kushiriki katika marasimu ya Arbaini ya Imam Hussein (as).
Taarifa hiyo imesisitiza kwamba, serikali ya Ufaransa ingali inaunga mkono na itaendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya hivi sasa ya Iraq kwa ajili ya kurudisha amani na utulivu katika nchi hiyo na kwamba itafanya juhudi kuhakikisha kwamba lengo hilo linafikiwa.
Siku ya Ijumaa, kundi moja la Waislamu wa Kishia waliokuwa njiani wakitembea kwa miguu ili kushiriki katika maombolezo hayo ambayo yanafikia kilele leo Jumatatu, lililengwa na magaidi huko kusini mwa Baghdad ambao walilipua bomu lililopelekea karibu watu 40 kupoteza maisha yao na wengine 80 kujeruhiwa. 364470