IQNA

14:42 - March 07, 2009
Habari ID: 1752794

Mufti wa Lebanon alaani dharau ya Wazayuni dhidi ya Mitume wa Mwenyezi Mungu

Mufti wa Lebanon ametoa taarifa akilaani hatua ya kanali ya 10 ya televisheni ya Israel ya kumvunjia heshima Mtume Muhammad (saw) na Nabii Issa Masih pamoja na mama yake Bibi Maryam (as).

Mufti Makki pia amelaani maandishi ya gazeti moja la Israel ambalo limetumia maneno ya maskhara kuhusu sira ya Imam Hussein (as). Amekitaja kitendo hicho kuwa ni kiovu na cha kuchukiza.
Amesema kuwa sira ya Imam Hussein ni miongoni mwa sira na historia zenye itibari kubwa mno.
Mufti wa kusini mwa Lebanon amewataka wafuasi wa dini za Kiislamu na Kikristo kuheshimu itikadi na matukufu ya pande hizo mbili na akasisitiza juu ya udharura wa kulinda hali ya maelewano kati ya wafuasi wa dini mbalimbali. 373579


captcha