IQNA

Kikao cha kitaifa cha Utamaduni na Urithi wa Tiba ya Kiislamu na Iran

18:30 - March 10, 2009
Habari ID: 1754502
Kitivo cha Elimu ya Tiba na Huduma za Afya cha Chuo Kikuu cha Beheshti kimeandaa kikao cha kwanza cha kitaifa cha Utamaduni na Urithi wa Tiba ya Kiislamu na Iran.
Kikao hicho kimefanyika kwa ushirikiano wa Wizara ya Afya, Tiba na Masomo ya Udaktari, Kamati ya Utamaduni na Ustaarabu wa Kiislamu na Iran ( Baraza Kuu la Mapinduzi ya Kiislamu) na Kituo cha Utafiti wa Maadili na Sheria za Udaktari.
Masuala yaliyojadiliwa katika kikao hicho ni kuhusiana na miongozo ya kitiba katika Uislamu, tiba ya jadi ya Iran, historia ya tiba ya Uislamu na Iran, mustakbali wa kunufaika na urithi wa kitiba na ushirikiano wa mataifa ya Kiislamu katika kuimarisha usalama wa jamii. 375330
captcha