Amesema kuwa ratiba hiyo ilianza kutekelezwa siku ya Jumatatu ambapo mipango mbalimbali ya kusherehekea kuzaliwa kwa Mtukufu Mtume (saw) imekuwa ikitekelezwa katika eneo hilo takatifu.
Wanazuoni na wanafikra mbalimbali wa Kiislamu wamepangiwa kutoa hotuba kuhusiana na masuala mbalimbali yanayohusiana na sifa na maisha ya Mtume na pia kuhusiana na Wiki ya Umoja katika siku hizo za kusherehekea kuzaliwa Mtume Mtukufu (saw).
Ratiba maalumu za kasida za kumsifu Mtume pia zitatekelezwa katika sherehe hizo. Ratiba zote zitakazotekelezwa katika haram hiyo zinaweza kufautiliwa moja kwa moja kupitia anwani ifuatayo: www.razavi.tv. 375967