Jarida hilo linajadili masuala mbalimbali yanayohusiana na maisha, kubaathiwa, malengo ya kupewa utume, majina, lakabu, maadili, tabia na miujiza ya Mtume Muhammad (saw).
Jarida hilo limejadili kwa undani maadili na tabia njema za Mtume Muhammad (saw), jambo lililochangia sana katika kuwafanya watu wakubali kwa haraka dini ya Uislamu.
Pamoja na kuwa inakubalika na wengi kwamba tabia hizo njema za Mtume ndizo zilizochangia kasi ya kuenea Uislamu katika pembe mbalimbali za dunia, lakini maadui wa dini hii tukufu wamekuwa wakieneza propaganda sumu dhidi yake kwa kutoa madai yasiyo na msingi kwamba dini hii inashajiisha utumiaji mabavu katika kufikia malengo yake. 375965