IQNA

11:50 - April 09, 2009
Habari ID: 1762320

Zawadi kwa wahudumu wa utamaduni wa Kiislamu nchini India

Duru ya pili ya kutunukiwa zawadi wahudumu wa utamaduni na utafiti wa Kiislamu ya Zawadi ya Shahid Muttahari ambayo hutolewa na Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini New Delhi nchini India itafanyika tarehe 30 Aprili katika ukumbi wa kitengo hicho.

Washindi wanne bora ambao wamewasilisha kazi nzuri za utafiti na uandishi wa Kiislamu watatunukiwa zawadi katika sherehe za kutolewa zawadi hizo ambazo zitafanyika sambamba na kuwadia siku ya kuuawa shahidi mwanafikra mashuhuri wa Kiislamu Ayatullah Murtadha Muttahari na ambazo zitahudhuriwa na shakhsia wa kielimu, kiutamaduni na kidini.
Mbali na kutunukiwa loho za shukrani, washindi pia watapewa zaidi ya fedha taslimu. 384947
captcha