Waziri huyo ameyasema hayo kwa mnasaba wa kuadhimishwa mwezi wa sanaa ya uigizaji nchini pamoja na Siku ya Kimataifa ya Sanaa. Amesema kuwa sanaa hiyo ni muhimu sana kwa taifa la Iran kwa sababu inabainisha, kufahamisha na kudhihirisha utamaduni wa mafundisho ya kijamii na kidini ya Wairani.
Safarharandi amesema kuwa athari za sanaa hiyo ya Iran zimekuwa zikionekana wazi katika ngazi za kimataifa pia, jambo ambalo ni dalili ya mafanikio makubwa ya sanaa ya uigizaji ya Iran. 391574