Waalimu wamegundua kuwepo makosa ya chapa katika nuskha moja ya Qur'ani iliyochapishwa mjini Damscus Syria, huko katika eneo la Jazan nchini Saudi Arabia. Walimu hao Khalid al-Jahni na Muhammad Nahari wa shule ya msingi ya Ahfad katika eneo la Jazan wamesema makosa hayo yalionekana katika baadhi ya sura ambapo jina la Mwenyezi Mungu limefutwa.